VIJANA WAMETAKIWA KUWA MSTARI WA MBELE KATIKA KAZI MBALI MBALI ZA JAMII NA KUJITOLEA KWA MOYO MMOJA KWANI VIJANA NDIO UTI WA MGONGO WA TAIFA

Vijana wametakiwa Kujua na Kufata taratibu na Sheria Za Barabarani Wakati Wa Kufanya Shughuli Mbali Mbali Za Usafilishaji Ilikuepuka Migogoro Na Wanao Simamia Sheria Za Barabarani.
Kauli Hiyo Imesemwa Na Mwenyekiti Wa Umoja Wa Vijana(UVCCM) Mkoa Wa Kigoma Bi Geraidina Kabululu Wakiambatana Na Mbunge Viti Maalum Kundi La Vijana Bi Silivia Sevula Wakati Wakiendelea Kupokea  Changamoto Mbali Mbali Za Waendesha Bodaboda Mkaoni Kigoma

Bi Kabululu Ameeleza Kuwa Changamoto Za Kukamatwa Kwa Boda Boda Wakiwa Katika Shughuli Zao Na Jeshi La Polisi Ni Tatizo Ambalo Linazungumzika na Tayari Wamekutana na pande Zote Mbili Ilikumaliza Tatizo Hilo Mkoani Kigoma.

Aidha Ziara Ya Mwenyekiti Wa Umoja Wa Vijana Mkoa Wa Kigoma Bi. Geraidina Kabululu Na Mbunge Kundi La VIjana Bi Silivia Sevula  Ya Kusikiliza Changamoto Mbali Mbali za Vijana Imeendelea Katika Wilaya Kasulu,Buhigwe,Kibondo Na Kakonko Mkaoani Kigoma.
Vijana Wametakiwa Kuwa Mstari Wa Mbele Katika Kazi Mbali Mbali Za Jami Na Kujitolea Kwa Moyo Mmoja Kwani Vijana Ndio Uti Wa Mgongo Wa Taifa 

 

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments