ANGELLAH KAIRUKI ASHIRIKI KONGAMANO LA UCHAGUZI, AMANI NA DUA JIJINI DAR ES SALAAM

 


 Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kibamba kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mhe. Angellah Kairuki, ameshiriki katika Kongamano la Uchaguzi, Amani na Dua lililoandaliwa na Baraza la Waislam Tanzania (BAKWATA) Wilaya ya Ubungo, Jimbo la Kibamba. Tukio hilo limefanyika katika Ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika kongamano hilo, Mhe. Kairuki amewahakikishia wananchi kuwa uchaguzi wa mwaka huu utakuwa wa amani, huku akisisitiza umuhimu wa kujitokeza kwa wingi kupiga kura ili kuchagua viongozi wanaowataka kwa hiari na utulivu.

Aidha, amewaomba masheikh na viongozi wa dini kuendelea kuhimiza amani, umoja na mshikamano miongoni mwa Watanzania kipindi chote cha uchaguzi.

Mhe. Kairuki pia amewasihi waumini wa Kiislam wa Jimbo la Kibamba pamoja na Watanzania kwa ujumla kumpigia kura za ndiyo Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kumpa kura nyingi yeye kama Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kibamba, pamoja na madiwani wote wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).







TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments