DKT.NCHIMBI AWASALIMIA WANANCHI WA JIMBO LA MANONGA, AMUOMBEA KURA DKT.SAMIA

Mgombea mwenza wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Emmanuel John Nchimbi akiwasalimia Wananchi wa Kata ya Ziba,Jimbo la Manonga,wakati akielekea kwenye mkutano wake wa jioni katika kata ya Ndala jimbo la Nzega Vijijini mkoani Tabora leo Oktoba 4, 2025.

Baada ya kuwasalimia wananchi hao,Dkt.Nchimbi aliwaomba pia kumpigia kura za ushindi wa kishindo Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani,Dkt.Samia Suluhu Hassan,aidha alimnadi mgombea Ubunge wa jimbo la Manonga,Ndugu Abubakari Alli Omari pamoja na Madiwani.

Balozi Nchimbi anafikia mkoa wa 18 sasa tangu kuzinduliwa kwa kampeni hizo Oktoba 28,2025 jijini Dar es Salaam,akiendelea kusaka kura za ushindi wa kishindo za Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan,Wabunge na Madiwani.








TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments