DUBE AIPA FURAHA YANGA!! WAWACHAPA AS FAR 1–0 ZANZIBAR

Mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga SC, wameendelea kutamba baada ya kuibuka na ushindi mwembamba wa bao 1–0 dhidi ya AS FAR Rabat katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika uliopigwa leo, Novemba 22, 2025, kwenye Dimba la New Amaan Complex, Zanzibar.

Bao hilo pekee lililowapa furaha Wananchi lilifungwa na mshambuliaji Prince Dube dakika ya 58, akimalizia kwa ustadi pasi murua ya kiungo Mudathir Yahya, ambaye alionesha ubunifu wa hali ya juu katikati ya uwanja.

Kwa matokeo hayo, Yanga SC imejikusanyia pointi tatu muhimu katika uwanja wao wa nyumbani, hatua inayowapa nafasi nzuri ya kujiongezea matumaini ya kusonga mbele kwenye hatua za juu za michuano hiyo mikubwa barani Afrika.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments