NCHI IMEPATA WAZIRI MKUU SAHIHI

 Baadhi ya wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wamesema kuwa uteuzi wa Dkt. Mwigulu Nchemba kuwa Waziri Mkuu, uliofanywa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ni uamuzi sahihi unaoonyesha dhamira ya kuhakikisha utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050 kwa weledi na ufanisi.

Wakizungumza nje ya viwanja vya Bunge mara baada ya Dkt. Mwigulu kuthibitishwa rasmi na Bunge kwa kura 369 kati ya kura 371, wabunge hao wamesema wana imani kubwa kuwa Waziri Mkuu huyo ataendelea kusimamia ipasavyo maendeleo ya nchi na kushughulikia changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi.

Mbunge wa Singida Magharibi (CCM), Elibariki Kingu, na Mbunge wa Simanjiro (CCM) James Ole Millya wamesema wanaaamini kuwa Dkt. Mwigulu atatoa kipaumbele katika kutatua changamoto za vijana, hususan tatizo la ukosefu wa ajira, ili kuhakikisha kundi hilo muhimu katika maendeleo ya taifa linanufaika na fursa zilizopo.

Wabunge hao wameongeza kuwa uteuzi huo ni uthibitisho wa uongozi makini wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuendeleza misingi ya uwajibikaji, utendaji bora na maendeleo endelevu kwa Watanzania wote.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments