MADIWANI WAMPIGIA KURA ZA HAPANA MGOMBEA PEKEE UENYEKITI HALMASHAURI MJI WA BARIADI

 Madiwani wateule kupitia chama cha mapinduzi (CCM) katika Halmashauri ya Mji wa Bariadi Mkoani Simiyu wamekataa kupitisha jina la Zebedayo Lazaro Kingi aliyeteuliwa na chama hicho kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo.

Katika uchaguzi huo wa kura za maoni ambao umefanyika leo, Mgombea huyo amepata kura 4 za ndiyo na kura za Hapana 11 kati ya kura 15 zilizopigwa.

Baadhi ya madiwani ambao wameshiriki uchaguzi huo (majina yanahifadhiwa) wamedhibitishwa matokeo hayo huku wakieleza kuwa Diwani huyo hakuwa chaguo lao.

“ Kamati ya siasa ilipendekeza majina mawili na hili la huyu likiwemo, lakini baada ya michakato ndani ya chama tukaletewa jina moja, ambapo tulitakiwa kupiga kura ya ndiyo na hapana, na huyu hakuwa chaguo letu tukaamua kupiga ya hapana, tumemkataa hatumtaki,” amesema mmoja wa Diwani.

Alipotafutwa na waandishi wa Habari Katibu wa CCM Wilayani Ibrahimu Kijanga ambaye alikuwa msimamizi wa uchaguzi huyo, amesema uchaguzi huo ilikuwa moja ya  michakato ya chama hicho ya ndani.

“ Siwezi kutoa matokeo, hii ilikuwa moja ya mchakato wa ndani ya chama chetu, tumemaliza uchaguzi na sasa tunaelekea katika hatua nyingine ndani ya chama,” amesema Kijanga.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments