Zingatia kuchimba dawa dakika 20 si 10

 

 MAMLAKA ya Udhibiti wa Usafiri Ardhini (LATRA), imeyataka mabasi ya usafirishaji mikoani kuzingatia muda wa kuchimba dawa kuwa ni dakika 20 badala ya 10.

Agizo hilo limetolewa jijini Arusha na Mkurugenzi wa LATRA, CPA Habibu Suluo katika Mkutano na waandishi wa habari.
“Kusimama eneo la huduma kwa walau dakika 20. Mambo ya kuchimba dawa dakika 10 hakuna.”

Amewataka wasafirishaji kutoacha abiria wakati kuchimba dawa, pia wazingatie usafi wa basi ikiwemo kumwagilia dawa za kuua wadudu pia kuweka vifaa vya kuhifadhi taka.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments