Hata hivyo watu wazima wanatakiwa waendelee kuvaa barakoa wanapokuwa maeneo ya ndani ya umma huku idadi maalumu ya watu wanaotakiwa kushiriki kwenye matukio yoyote ya pamoja ikiendelea pia kuhimizwa nchini humo.
Takwimu rasmi za serikali ya Afrika Kusini zinaonesha kuwa watu milioni 3.8 wamekumbwa na ugonjwa wa UVIKO-19 nchini humo huku idadi ya waliofariki dunia ikiripotiwa kuwa ni watu 100,407. Idadi hiyo ni kubwa zaidi katika bara zima la Afrika. Sasa hivi zaidi ya asilimia 45 ya watu wazima wameshapiga chanjo kamili ya corona nchini Afrika Kusini.
![]() |
Raia wa Afrika Kusini akipiga chanjo ya corona |
Baada ya kupungua kidogo maambukizi ya corona mwezi uliopita idadi ya watu waliokumbwa na ugonjwa huo ilipanda tena juzi Jumatano. Zaidi ya wagonjwa wapya 6,100 wa corona waliripotiwa nchini Afrika Kusini.
Idadi ya watu wanaoruhusiwa kukusanyika pamoja katika maeneo ya ndani nchini humo mwisho ni 1,000 au nusu ya idadi yoyote ya watu wanaoweza kuingia kwenye eneo husika la ndani lililofungwa kila upande.
0 Comments