Man United mwaka wa tabu

TIMU ya Manchester United imeaga michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kumaliza kundi A ikiwa na pointi nne, ambazo zimeshindwa kuwavusha kwenda 16 bora.

Katika mchezo wa leo dhidi ya Bayern Munchen ulioisha kwa United kufungwa bao 1-0, timu hiyo ilihitaji ushindi wowote kisha Copenhagen na Galatasaray wamalize kwa sare ila mambo yakawa tofauti baada ya Copenhagen kushinda bao 1-0.

Kwa matokeo hayo, Bayern Munchen imeenda 16 bora ikiwa na pointi 14, na Copenhagen ikiwa na pointi 8.

United ilianza kundi hilo kwa mchezo dhidi ya Bayern ambapo waliofungwa mabao 4-3, kisha wakafungwa tena dhidi ya Galatasaray mabao 3-2.

Mchezo wa tatu dhidi ya Copenhagen, United walishinda bao 1-0, katika mchezo wa marudiano dhidi ya timu hiyo, wakapoteza tena mabao 4-3. United walipata sare ya mabao 3-3 dhidi ya Galatasaray mchezo wa marudiano.

Katika mchezo wa leo, bao la Bayern limefungwa na Kingsley Coman dakika ya 70.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments