WAATHIRIKA WA MAFURIKO MVOMERO WAGAWIWA VIWANJA

Kufuatia Mvua zinaendelea kunyesha mkoani Morogoro Mkuu wa wilaya ya Mvomero ameiagiza halmashauri ya wilaya hiyo kuhakikisha inagawa haraka viwanja kwa waathirika wa mafuriko yaliyotokea wilayani humo kata ya Mvomero ambapo zaidi ya watu 500 wanaokadiriwa kukoswa maakazi kwa sababu ya mafuriko.

🔴LIVE: Ziara ya Katibu wa NEC Itikadi, Uenezi na Mafunzo Ndugu Paul C. Makonda Mkoani Tabora

DC Nguli ametoa maagizo hayo wakati alipotembelea baadhi ya maeneo yaliyoathiriwa na mvua ambazo zimeleta athari kubwa ikiwemo nyumba zao kubomoka jambo lililosababisha Wananchi hao kukosa makazi pamoja na huduma za kijamii.

Kwa upande wake mwakilishi wa bodi yamaji ya bonde la Wami Ruvu Antony Lugai amesema chanzo cha maji haya ni baadhi ya mito kujaa michanga hivyo kushindwa kupeleka maji kwenye mkondo unaotakiwa jambo lililosababisha maji kuelekea katika makazi ya watu.

#VIDEO: Wananchi Mkoani Singida Wametakiwa Kuendelea Kutoa Taarifa Kwa Jeshi La Polisi

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments