WIZARA YA KILIMO KUSAMBAZA ZAIDI YA TANI 2000 ZA MBENGU ZA ALIZETI NCHIN...

                                   
                  
Naibu Waziri wa Kilimo DAVID SILINDE amesema Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na Wakala wa Mbegu - ASA imeanza kusambaza Mbegu Bora za Alizeti Zaidi ya Tani 2,000 zenye Ruzuku kwa Wakulima nchi nzima kwa Msimu wa Kilimo 2023/2024.

 

Naibu SILINDE ametoa taarifa hiyo wakati akizundua zoezi la Usambazaji wa Mbegu Bora za Alizeti zenye Ruzuku kwa wakulima wa Mkoa wa Singida ambapo Mkoa wa Singida kwa msimu huu utapokea Tani 600 za Mbegu.

 

Amesema tangu Wiraza ianza utaratibu wa kusambaza Mbegu Bora za Alizeti Uzalishaji umeongezeka hivyo akaziagiza Halmashauri kutoa ushirikiano kwa Wizara na Wakala wa Mbegu ili zoezi la usambazaji wa Mbegu Bora za Alizeti liweze kufanikiwa kwa kuwafikia wakulima wote.

 

Pamoja na kuwataka wakuu wa Wilaya kwenda kusimamia suala la usambazaji wa Mbegu amewataka Viongozi kwenda kusimamia makubaliano ya Serikali ya Mkoa ya kuanzisha Mfumo wa Stakabadhi Ghalani kwa lengo la kuwasaidia wakulima kuuza mazao yao kwa bei halali.

 

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba alitoa maelekezo kwa Wakulima kutumia Mbolea kwenye mashamba yao ili waongeze Uzalishaji.


MATUKIO MBALI MBALI YA PICHA













KUTOKA SINGIDA



TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments