GGML YAZINDUA MPANGO WA MAFUNZO KAZINI KWA MWAKA 2024/2025, WANAFUNZI 40 KUFAIDIKA

 


Makamu Rais Mwandamizi - Kitengo cha Biashara Afrika, Terry Strong akizungumza katika hafla ya kuwakaribisha wanafunzi hao.
Wahitimu 40 wa vyuo mbalimbali nchini ambao wanatarajia kuanza mpango wa mafunzo kazini kwa vitendo unaodhaminiwa na kampuni ya GGML kwa mwaka 2024/2025 wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kukaribishwa rasmi mwishoni mwa wiki mkoani Geita. 

NA MWANDISHI WETU
KATIKA kudhihirisha dhamira ya kuwajengea wahitimu wa vyuo mbalimbali kukubalika kwenye soko la ajira, Kampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imezindua mafunzo tarajali kwa wanafunzi 40 waliohitimu vyuo mbalimbali nchini.

Mafunzo hayo yanayotolewa kwa muda wa mwaka mmoja (2024/2025), yatahusisha programu mbalimbali ikiwamo za uanagenzi, mafundi mchundo, watalaam wa masuala ya madini ya fani nyingine ambazo zimeanzishwa ili kukuza ujuzi wa vijana wa kitanzania.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments