TCRA yatoa WiFi ya dezo msibani

 

ARUSHA: Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imetoa huduma ya Internet bure (WiFi) katika kijiji cha Ngarash wilayani Monduli nyumbani kwa Hayati Edward Lowassa.
 
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Dk Jabiri Bakari akizungumza amesema wamerahisisha shughuli ya mawasiliano kwa waombolezaji ili wasipate tabu katika kuwasiliana.
 
“Maeneo haya kumekuwa na watu wengi kwa gafla, tumeongea na watoa huduma wa mitandao ya simu wa ‘adjust’ huduma za mitambo yao ile lodi itakayokuwepo hapa itaweza kubebwa,”amesema Jabiri na kuongeza
 
“TTCL tayari imeshasogeza ‘fiber’ ili kupunguza lodi kwenye mitandao ikiwemo data, kutakuwa na free WiFi kwa waombolezaji.”amesema
 
Mwili wa Lowassa umeshawasili Monduli na maziko yanatarajiwa kuwa siku ya Jumamosi.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments