‘Tumejiandaa vizuri kumkabili mnyama’

TABORA: NAHODHA wa Tabora united, Saidi Mbatty amesema kuwa wachezaji wote katika kikosi chao wamejiandaa vyema kuikabili Simba SC katika mchezo utakaochezwa Februari 06, 2024, Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, mkoani Tabora.

Akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari leo, Mbatty amesema wanafahamu fika Simba ni timu kubwa na ina wachezaji wazuri lakini maandalizi yao ni kuzisaka pointi tatu.

“Sisi kama Tabora United tumejiandaa kwenye mchezo wa kesho na tuna deni kubwa kwa wana tabora kwa sababu kila tunapocheza kwenye Mkoa wetu wanakuja kutusapoti hivyo tunajua tunaenda kufanya nini siku ya kesho hivyo tunawaomba waje kwa wingi siku ya kesho.” Amesema.

Nahodha huyo ameongeza kuwa katika mchezo wa kesho watazingatia zaidi maelekezo ya mwalimu na benchi la ufundi kwa ujumla ili waweze kuvuna pointi tatu licha ya mpinzani wake kuibuka na ushindi wa 1-0 dhidi ya Mashujaa fc wakiwa katika Uwanja wao wa nyumbani.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments