Yanga tatu nyingine, Mudathir wa moto

MOROGORO: Yanga imeendelea kujichimbia kileleni mwa Ligi kuu Tanzania bara baada ya kuitandika KMC 3-0 kwenye mchezo uliomalizika muda mchache uliopita Uwanja wa Jamhuri mkoani Morogoro.

Matokeo hayo yameifanya Yanga kufikisha alama 43 katika michezo 16 walioshuka dimbani msimu huu na kuongeza wigo wa tofauti ya alama baina yake na Simba wanaoshika nafasi ya pili wakiwa na alama 36.

Magoli ya Yanga katika mchezo huo yamefungwa na kiungo Mudathir Yahya aliyeingia kambani mara mbili dakika ya 01 ,54 na Pacome Zouzoua aliyepigilia msumari wa tatu na wa mwisho dakika ya 59 ya mchezo.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments