Hospitali tano zavunja mkataba wa NHIF

DAR ES SALAAM: Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) umewataka wananchama wake kutumia vituo vya afya mbadala baada ya hospitali tano za Kairuki, TMJ, Apollo, Aga Khan na Regency kuvunja mkataba wa utoaji wa huduma baina yao na Mfuko.

Taarifa ya NHIF imesema Maofisa wake watakuwa katika vituo hivyo kuhakikisha wanachama wenye changamoto za tiba wanapata msaada katika vituo vingine.

Anjela Mziray, Meneja Uhusiano wa NHIF amesema leo Machi 1 kuwa Mfuko huo unaendelea kufanya usajili wa vituo vingine binafsi ili kuongeza wigo wa watoa huduma na kusogeza kuduma kwa wanachama.

 

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments