Ronaldo afungiwa mechi moja, faini

 

RIYADH, Saudi Arabia: CRISTIANO Ronaldo amefungiwa mechi moja kwa kosa la kufanya kitendo kinachodaiwa kuwa cha kuudhi wakati wa mchezo wa ligi ya Saudi Arabia kati ya Al Nassr na Al-Shabab.

Baada ya Al-Nassr kushinda 3-2 Jumapili, picha za video zilimuonesha Ronaldo akionesha ishara ya kuwasikiliza mashabiki na kuchezesha mkono wake karibia na nyonga, ishara iliyoonekana kuwalenga mashabiki wa Al-Shabab.

Kamati ya Nidhamu na Maadili ya Shirikisho la Soka la Saudi Arabia (SAFF) ilitangaza adhabu hiyo kwenye mitandao ya kijamii leo Alhamisi.

Mechi inayofuata ya ligi ya Al-Nassr itakuwa nyumbani dhidi ya Al-Hazm leo.

Nyota huyo wa zamani wa Real Madrid na Manchester United pia atalazimika kulipa faini ya Saudi Riyal 20,000 ($5,333) kwa Al-Shabab, ili kulipia gharama za klabu hiyo kuwasilisha malalamiko hayo, na nusu ya kiasi hicho kwa shirikisho hilo.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments