Azimio hili limetolewa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Husna Sekiboko, alipokuwa akiwasilisha taarifa ya shughuli za kamati hiyo kwa mwaka wa fedha 2024 hadi 2025, katika kikao cha Bunge kilichofanyika leo Februari 11, 2025 jijini Dodoma.
Katika hatua nyingine, Sekiboko aliipongeza serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuongezea bajeti wizara za Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na Habari, Utamaduni na Michezo, jambo lililosaidia kufanikisha utekelezaji wa miradi mingi kwa ufanisi.
Hata hivyo Sekiboko , aliiomba serikali kuhakikisha inatekeleza miradi inayoendelea kwa wakati ili kuleta maendeleo ya haraka kwa Taifa na Jamii kwa ujumla.


0 Comments