"Kauli ya Msita Yazua Mjadala: 'Tusikimbiane Kama Tarehe 8'’

                       
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC) kutoka Mkoa wa Singida, Yohana Msita, ametoa wito kwa wananchi kudumisha amani na mshikamano, akisisitiza kuwa taifa halipaswi kurudia taharuki iliyotokea tarehe 8 mwezi wa tatu 2025. Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika Kata ya Ipande Jimbo la Itigi Wilayani Manyoni Mkoani Singida

Katika hotuba yake, Msita alisema, "Tusikimbiane kama tulivyofanya tarehe 8. Tukumbuke kuwa amani ni msingi wa maendeleo. Hakuna sababu ya kuruhusu hofu kutawala tena miongoni mwetu." Hata hivyo, hakufafanua moja kwa moja kilichotokea tarehe hiyo, lakini kauli yake ilionekana kuelekezwa kwa matukio ya kimechezo yaliyowahi kuvuruga utulivu katika baadhi ya maeneo.

Alisisitiza kuwa chama chake kipo tayari kusikiliza maoni ya wananchi na kushirikiana katika kuleta maendeleo ya kweli kwa kila Mtanzania. Aliwataka viongozi wa kisiasa kutumia majukwaa yao kuhubiri umoja badala ya uchochezi unaoweza kuchochea migawanyiko.

Wananchi waliokuwa wamehudhuria mkutano huo walionekana kuguswa na kauli hiyo, huku baadhi wakieleza kuwa ni muhimu kwa viongozi wote wa kisiasa kutoa kauli za kutuliza hali badala ya kuibua hisia kali miongoni mwa wananchi.

                                     

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments