MCHENGERWA AOMBA RIDHAA KWA CCM KUGOMBEA UBUNGE WA RUFIJI

 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais- TAMISEMI na aliyekuwa Mbunge wa Rufiji Mhe. Mohamed Mchengerwa leo Juni 30, amejitokeza kuomba ridhaa kwa Chama chake- Chama cha Mapinduzi (CCM) kuchaguliwa kuwa mgombea ubunge wa jimbo hilo katika Uchaguzi Mkuu wa Mwezi Oktoba mwaka huu.

Mhe. Mchengerwa amefika kwenye ofisi ya Wilaya ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Rufiji katika Mji wa Utete kilomita takribani 60 kutoka barabara kuu ya Dar es Salaam - Lindi kuchukua na kisha kukabidhiwa fomu ya kuomba ridhaa kutoka kwa Katibu wa CCM Wilaya ya Rufiji na baada ya kukamilisha taratibu zote akairejesha.

Mhe. Mchengerwa aliambatana na mama yake mzazi, ambapo baada ya kuwasilisha fomu asema ameamua kutumia haki ya kuchagua na kuchaguliwa ili aendelee kuwaletea maendeleo wananchi wa Rufiji na kisha akaondoka.




TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments