“CCM Inatekeleza – Mgonto Anaendeleza!” Uzinduzi wa Kmpeni jimbo la Ikungi Mashariki.

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Ikungi Mashariki kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Chief Thomas Mgonto, ameonyesha dhamira ya dhati ya kuendeleza kasi ya maendeleo katika jimbo hilo, akisisitiza utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa kuzingatia mahitaji halisi ya wananchi katika kila eneo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni za uchaguzi jimboni humo, Chief Mgonto alibainisha kuwa dhamira ya CCM ni kuwatumikia wananchi kwa kuzingatia maslahi ya jamii na taifa kwa ujumla.

 Amesema kipaumbele chake ni kuhakikisha kila sekta muhimu—elimu, afya, barabara, kilimo na maji—inaendelea kupiga hatua ili kuongeza ustawi wa wananchi wa Ikungi Mashariki.

Aidha, Mgonto amewataka wananchi kuendelea kuiamini CCM kwani ndiyo chama pekee chenye historia, uzoefu na uthubutu wa kuwaletea maendeleo ya kweli.

 Pia aliwahimiza kumpigia kura mgombea urais kupitia CCM, wabunge na madiwani, akisema viongozi bora na wenye kuenzi amani ya taifa wanatokana na CCM.

Wananchi walipokea kwa hamasa kubwa ujumbe wa Mgonto, wakiahidi kumpa ushirikiano ili kuendeleza kazi kubwa ya maendeleo iliyofanywa na serikali ya awamu ya sita.

Matukio kwa Picha 






Alifu Abdul Singida Ikungu

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments