LIVERPOOL YACHANA MKEKA ANFIELD

JURGEN Klopp, Kocha Mkuu wa Liverpool amesema kuwa wachezaji wake walitengeneza nafasi nyingi kwenye mchezo wao wa Merseyside Derby dhidi ya Everton licha ya kupoteza kwa kufungwa mabao 2-0.


Kwenye mchezo huo uliochezwa Uwanja wa Anfield, nahodha wa Liverpool, Jordan Henderson hakuweza kumaliza dakika 90 kwa kuwa aliumia msuli na nafasi yake ilichukuliwa na Nat Phillips jambo ambalo linaongeza orodha ya majeraha ndani ya kikosi hicho.

 Nyavu za Liverpool ambazo zimekosa huduma ya kitasa wao Virgil van Dijk kutokana na kusumbuliwa na majeraha zikitikiswa na Richarlison dakika ya 3 na ule wa mwisho mtikisiko ulikuwa dakika ya 83 kwa mkwaju wa penalti uliopigwa ba Gylfi Sigurasson.

Dakika 90 zilikamilika kwa mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu England kupiga jumla ya mashuti 15 na sita yalilenga lango huku wapinzani wao Everton wakipiga jumla ya mashuti 9 na sita yalilenga lango.

Mbali na hilo pia umiliki wa mpira kwa Liverpool iliyo nafasi ya 6 na pointi 40 baada ya kucheza mechi 25 ilikuwa ni asilimia 72 huku Everton iliyo nafasi ya 7 na pointi 40 abaada ya kucheza jumla ya mechi 24 ikiwa ni asilimia 28.

Klopp amesema:"Tulicheza vizurri kwenye umiliki pia ilikuwa hivyo hata kushambulia kwetu ilikuwa zaidi yao ila vijana wameshindwa kutumia nafasi, hakuna namna tunajipanga kwa ajili ya wakati ujao,".

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments