Majaliwa: Wazazi wapunguzieni watoto majukumu wapate muda wa kusoma



Dar es Salaam. Waziri mkuu wa Tanzania,  Kassim Majaliwa amewataka wazazi na walezi kuhakikisha  wanawapunguzia watoto majukumu ya  nyumbani ili  kuwawezesha kupata muda wa kujisomea na kupumzika.

Majaliwa amesema hayo leo Jumanne Februari 23, 2021 wakati akizungumza na walimu, wanafunzi na wazazi baada ya kukagua miundombinu ya shule ya msingi Mitope, Ruangwa mkoani Lindi.

Amesema iwapo watoto watapata muda mzuri wa kujisomea na kupumzika itawasaidia  kuwaongezea ufaulu kwenye masomo yao na kutimiza ndoto zao.

Mbali na hilo, Majaliwa  amewataka wazazi na walezi kuhakikisha wanafunzi wananunuliwa vifaa vyote vinavyohitajika shuleni  zikiwemo  sare, madaftari sanjari na kufuatilia mienendo yao kielimu.

”Wazazi tufuatilie na kujiridhisha kama watoto wetu wanafika shule na kuingia madarasani. Pia tuwe tunakagua madaftari yao na pale tunapoona hawafanyi vizuri tuwasiliane na walimu,” amesema Majaliwa.

Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa, Hashim Mgandilwa amesema atahakikisha anashirikiana na viongozi wenzake kuendelea kusimamia vizuri shughuli za maendeleo.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments