Viongozi wamlilia Makamu wa kwanza wa Rais Zanzibar Maalim Seif

 Dar es Salaam. Ni simanzi. Ndivyo unavyoweza kusema baada ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad kufariki dunia leo Jumatano Februari 17, 2021 katika hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) alikokuwa akipatiwa matibabu.

Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi ametangaza siku saba za maombolezo huku Rais John Magufuli naye akitoa salamu za pole.

Viongozi mbalimbali pia wametuma salamu za rambirambi kufuatia kifo cha mwenyekiti huyo wa chama cha ACT-Wazalendo ambaye kabla ya kujiunga na chama hicho alikuwa katibu mkuu wa CUF.

Kupitia kurasa za mitandao ya kijamii Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Mwigulu Nchemba amesema, “pumzika kwa amani mzee wetu Maalim Seif, makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar. Natoa pole kwa familia, Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar na Watanzania wenzangu wote. Pumzika kwa Amani.”

Mwanasheria Fatma Karume amesema, “inna lilahi wa inna ilayhi rajiun Nimehuzunika sana kusikia Maalim amefariki. He was a good man and a good friend.”

viongoziwamliliapic
Mwanaharakati Maria Sarungi ameandika, “kwa msiba huu mzito! Poleni Wazanzibari na pole zetu Watanzania na Tanzania kama Taifa! This is absolutely devastating news! Tumeumia sana! Inna Lillahi wa inna ilayhi rajun Maalim Seif.”
Katibu mkuu wa Chadema, John Mnyika amesema amepokea kwa masikitiko kifo cha Maalim Seif na kwamba ni pigo kwa Taifa kwa kupoteza kiongozi shupavu.

Kwa upande wake kiongozi wa chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe alinukuu maneno aliyozungumza Maalim Seif mwaka 1987 katika viwanja vya Tibirizi mjini Pemba.

viongoziiipic

 Nipo nanyi sasa hivi, ninawaahidi kuwa nitakuwa nanyi nikiwa ndani ya Serikali au nje ya Serikali. Nitakuwa nanyi nikiwa ndani ya chama au nje ya Chama.”

 Seif Sharif Hamad, Desemba 1987 Viwanja vya Tibirinzi, Pemba – Zanzibar.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments