Wabunge wataka changamoto za muungano kutatuliwa kwa wakati

Mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria, Joseph Mhagama akiwasilisha bungeni maoni ya kamati hiyo kuhusu makadirio ya mapato na matumizi ya Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) kwa mwaka wa fedha 2021/2022, jijini Dodoma leo. Picha na Edwin Mjwahuzi

Dodoma. Wabunge nchini Tanzania wameitaka Serikali ifanye jitihada za ziada katika kuhakikisha changamoto za kifedha na za kikodi zinazolalamikiwa na wananchi wa pande zote mbili za Muungano, zinapatiwa ufumbuzi kwa wakati.

Jana Makamo wa Rais Dk Philip Mpango wakati akifungua kongamano la miaka 57 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar bila kuzitaja alisema changamoto 15 kati ya 25 za muungano zilitatuliwa.

Mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria Joseph Mhagama ameyasema hayo leo Jumanne Aprili 27, 2021 wakati akitoa maoni yake katika makadirio ya mapato na matumizi ya ofisi ya Makamo wa Rais Muungano na Mazingira.

Amesema kamati inaendelea kushauri Serikali ifanye jitihada za ziada katika kuhakikisha changamoto za kifedha na za kikodi zinazolalamikiwa na wananchi wa pande zote mbili za Muungano, zinapatiwa ufumbuzi kwa wakati.

Amesema hatua ambayo itachochea ukuaji wa uchumi kwa mwananchi mmoja mmoja na kwa manufaa ya Serikali zote mbili.


Aidha, Serikali iendelee na juhudi hizo katika  kubaini changamoto mpya zinazoweza kuibuka na kuzitatua kwa haraka.


TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments