MWANA FA AELEZEA AJALI ALIYOPATA


Mbunge wa jimbo la Muheza Hamis Mwinjuma maarufu Mwana FA
***
Mbunge wa jimbo la Muheza Hamis Mwinjuma maarufu Mwana FA, amepata ajali ya gari eneo la Mkambalani mkoani Morogoro jana Agosti 31, 2021 usiku.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro Fortunatus Muslim na kueleza kuwa mbunge huyo yupo salama.

Kwa upande wake Mwana FA alipopata nafasi ya kuongea na waandishi wa habari alieleza kuwa kabla ya ajali waliona gari mbele yao inataka kupita gari (Overtake) na ilikuwa mwendokasi sana hivyo hawakuweza kuikwepa ndio ikawaparamia.

Picha kutoka eneo la ajali

Aidha amesema kiafya yeye na mwenzake aliyekuwa naye kwenye gari ni wazima ila alikuwa anasikia maumivu kidogo kifuani mwake.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments