Zijue siku zako za hedhi kuilinda ngozi ya uso

Licha ya kufanya vitu kadha wa kadha kulinda ngozi isiharibike, kuna sababu za kimaumbile, ikiwamo mabadiliko ya homoni ambayo huifanya ngozi kubadilika na wakati mwingine kupata chunusi.

Soma hapa: Mambo gani wanawake watarajie wanapokaribia kukoma hedhi

Hili hutokea kwa baadhi ya wanawake kila mwezi wanapokuwa kwenye hedhi. Ili kukabiliana na hali hii, unapaswa kuhakikisha unajua tarehe unazopata hedhi. Ukijua tarehe za kupata hedhi, zikikaribia

kanda uso kwa mvuke.

Yaani chemsha maji yaweke kwenye chombo kipana kama beseni kisha jifunike nguo nyepesi ili kupata mvuke,

Soma hapa: Fahamu mzunguko sahihi kwa mwezi

hakikisha hayana moto sana ili kuepuka kubabuka. Kama una mashine ya mvuke unaweza kuitumia, mara nyingi zinakuwepo kwenye saluni za kiume.

Ikiwezekana pia osha uso mara mbili kwa siku kwa sabuni unayoitumia, pia usilale na vipodozi na ukiweza punguza kutumia vyenye mafuta.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments