HII HAPA RATIBA YA LIGI KUU BARA LEO SEPTEMBA 28

SEPTEMBA 28, Ligi Kuu Bara inaendelea kuchanja mbuga baada ya jana Septemba 27 kuanza kasi kwa timu tatu kupambana kusaka pointi tatu. 

Simba inayonolewa na Kocha Mkuu,  Didier Gomes itakuwa Uwanja wa Karume, Mara bila uwepo wa nyota wao Taddeo Lwanga ambaye alionyeshwa kadi nyekundu katika mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Yanga, Uwanja wa Mkapa, Septemba 25.

Mbali na mchezo huo unaosubiriwa kwa shauku kubwa pia Dodoma Jiji itakuwa na kibarua cha kusaka pointi tatu mbele ya Ruvu Shooting,  Uwanja wa Jamhuri, Dodoma. 

Pia kuna mchezo mwingine ambapo Mbeya City itakuwa na kibarua cha kusaka pointi tatu mbele ya Tanzania Prisons,  Uwanja wa Sokoine.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments