JUKWAA LA WANAWAKE MKURANGA WAPATA MWENYEKITI, WAKABIDHIWA CHEREHANI SABA

JUKWAA la Wanawake Wilaya Mkuranga mkoani Pwani wamemchagua Mariam Ulega kuwa Mwenyekiti wao baada ya kuibuka na ushindi wa kura 99 dhidi ya kura saba alizopata mshindani wake.

Akizungumza baada ya kutangazwa kushinda nafasi ya Mwenyekiti wa Jukwaa hilo,Mariam Ulega ameahidi kufanya kazi za kwa bidii,juhudi na maarifa na kwamba hatawaangusha wanawake wa Mkuranga.

"Nitahakikisha nashirikiana  wananchi wote wa Mkuranga katika kuendelea kuleta maendelo .Nitahakikisha nasimama imara katika kuifanya Wilaya yetu inapaa kimaendeleo,"amesema Mariam Ulega.

Amewaomba wanaweke ambao hawana vikundi  wavianzishe na kisha wavisajali na hatimaye kukopeshwa fedha ambazo hazina riba kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga, na hivyo wataweza kuinuka kiuchumi kwa kufanya shughuli mbalimbali.

Mbali ya kutoa shukrani kwa wapiga kura wa jukwaa hilo,Mwenyekiti huyo amesema Jukwaa hilo la Wanawake Mkuranga wamepokea Cherahani saba kutoka kwa Mbunge wa Jimbo la Mkuranga,Abdallah Ulega.

"Leo tumepolea Cherehani saba kutoka kwa Mbunge , ni vema  tuzitunze  na zifanye kazi iliyokusudiwa ya kushona nguo za watoto wa shule , uwepo wa Cherehani hizo zitawezesha wakina mama wa Mkuranga tusonge mbele,"amesema.Mwenyekiti wa Jukwaa la Wanawake Wilaya ya Mkuranga,Mariam Ulega  akizungumza na wapigakura baada ya kutangazwa kushinda nafasi ya Mwenyekiti wa Jukwaa hilo, ambapo ameahidi kufanya kazi kwa bidii,juhudi na maarifa na kwamba hatawaangusha wanawake wa Mkuranga.Uchanguzi  huo umefanyika leo  kwenye ukumbi wa Parapanda  Wilaya ya  Mkuranga Mkoani wa Pwani.(Picha na Emmanuel Massaka wa Michuzi TV)Mwenyekiti wa Jukwaa la Wanawake Wilaya ya Mkuranga,Mariam Ulega (kushoto) akimkabidhi Cherehani Makamu Mwenyekiti wa Jukwaa hilo.

Wanawake wakishangilia  ushindi wa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wanawake Wilaya ya Mkuranga,Mariam Ulega kama wana  wanavyoonekana pichani.(Picha na Emmanuel Massaka wa Michuzi TV)

Sehemu ya wapiga kura  wakiburudika katika Ukumbi wa  Parapanda  Wilaya ya  Mkuranga Mkoani wa Pwani.
Mwenyekiti wa Jukwaa la Wanawake Wilaya ya Mkuranga,Mariam Ulega  (wapili kushoto) akiwa kwenye picha ya mamoja na wapikura.

Mwenyekiti wa Jukwaa la Wanawake Wilaya ya Mkuranga mkoa wa Pwani,Mariam 

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments