MARUFUKU MACHINGA KUFANYA BIASHARA KWENYE NJIA ZA WATEMBEA KWA MIGUU - RC MAKALLA

 






-  Wamachinga wakiri kuingilia maeneo ya watembea kwa miguu na kuahidi kuhama

- Aeleza dhamira yake ya kuboresha mandhari ya Dar es salaam

MKUU wa Mkoa wa Dar es salaam  Amos Makalla amepiga marufuku ufanyaji wa biashara kwenye maeneo hifadhi ya barabara zote za Mkoa huo baada ya utaratibu huo kuwa chanzo cha uvunjifu wa amani na ongezeko la ajali.

RC Makalla ametoa maelekezo hayo alipotembelea Soko la Kariakoo na kujionea kero ya ufanyaji biashara holela kwenye maeneo ya watembea kwa miguu.

Kutokana na hilo RC Makalla amewaelekeza Mkuu wa Wilaya ya Ilala kufanya kikao na Wafanyabiashara hao Jumatatu ya Septemba 13 na kuainisha maeneo ya kuwapeleka wote waliovamia hifadhi ya barabara.

Aidha RC Makalla amewaelekeza kuangalia utaratibu mzuri wa kufunga na kufungua baadhi ya mitaa Kariakoo kwaajili ya kufanya biashara Kutokana na ufinyu wa maeneo ili Waweze kupata riziki.

Hata hivyo RC Makalla amesema kwa tathimini aliyofanya amebaini hali ya ufanyaji biashara holela Dar es salaam ipo kwa kiwango kikubwa na kuwanyima watembea miguu haki zao za msingi.

Pamoja na hayo RC Makalla ameelekeza Manispaa zote za Mkoa huo kuweka vibao vya kuzuia biashara kwenye maeneo ya watembea kwa miguu.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments