Mikasa 9 ya kibabe ya Hans Poppe Simba

 


NI msiba wa wanamichezo kutokana na kifo cha aliyekuwa Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi Simba, Zacharia Hans Poppe ambaye roho yake iliacha mwili usiku Septemba 10, 2021.

Umauti wa Hans Poppe umemkuta akiwa Hospitali ya Aga Khan, jijini Dar es Salaam akiwa anapigania afya yake baada ya kupumzishwa hapo kwa takribani wiki mbili.

Ndani ya Simba Hans Poppe alikuwa na nguvu kubwa, kwa sasa unaweza kusema ukimwondoa Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Mohammed Dewji ‘MO’ na makamu wake Salim Abdallah ‘Try again’ basi anayefuata alikuwa Hans Poppe.

Hapo nyuma kabla ya ujio wa MO Hans Poppe ndio alikuwa alfa na omega, ndani ya Simba alikuwa hachoki kutumia fedha zake kuhakikisha Simba inakaa sawa sawa, lakini baadaye baada ya kuja kwa mabadiliko ya kiuongozi baada ya mchakato wa uwekezaji, hapo ndipo kijiti alipokipokea MO na Try again na yeye akibaki kuwa mjumbe ingawa bado alikuwa na nguvu yake.

Hebu tuangalie matukio ya kibabe ambayo Hans Poppe alikuwa akiyafanya enzi za uhai wake ndani ya klabu ya Simba aliyoipigania mchana na usiku kuhakikisha inakaa sawa.


TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments