RC MAKALLA: HAKUNA KUZUIA MAITI KWA KIGEZO CHA DENI.

 - Ataka Wafiwa wapewe mwili wakazike.


-Awaonya wanaokiuka Maelekezo na Tamko la Wizara.

- Ataka Maiti kuheshimiwa.

- Awaelekeza Waganga Wakuu wa Wilaya kuhakikisha upatikanaji wa dawa muhimu za Wazee.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Amos Makalla amepiga marufuku hospitali kuzuia maiti kwa sababu mgonjwa alishindwa kulipa deni na badala yake wakabidhi mwili kwa Ndugu wa marehemu kwaajili ya kuzika wakati taratibu nyingine zinaendelea.

RC Makalla ametoa maelekezo hayo baada ya kupokea Malalamiko ya Wananchi juu ya baadhi ya hospital Mkoani humo kuendelea na utaratibu wa kuzuia maiti licha ya Serikali kupitia Wizara ya Afya kukataza uzuiaji wa maiti.

Kutoka na hilo RC Makalla amewaelekeza Waganga Wakuu wa Wilaya Chini ya Wakuu wa Wilaya kuhakikisha tatizo hilo halijirudii Katika Maeneo yao.

Aidha RC Makalla amewaelekeza Waganga Wakuu wa Wilaya kuhakikisha wanazingatia suala la Matibabu kwa Wazee ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa dawa muhimu kwaajili ya Wazee.

Hayo yote yamejiri wakati wa Mwendelezo wa ziara ya kusikiliza na kutatua Migogoro ya Wananchi Jimbo la Kinondoni.


TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments