RAIS SAMIA: TUTATUE KERO ZINAZOWAKABILI WAWEKEZAJI

Rais Samia Suluhu Hassan amewataka watendaji wa Serikali kuweka utaratibu wa kufuatilia kero zinazowakabili wawekezaji na kuzitatua.


Mhe. Rais ametoa agizo hilo leo alipokuwa katika ziara ya kikazi katika Wilaya ya Longido, Mkoa wa Arusha.“Tunavuta wawekezaji wanakuja lakini wakifika na wakishajenga viwanda, tusiwaache wenyewe, tufuatiliena tujue kero zinazowakabili na tuzitatue,” ameagiza Rais Samia.

Tangu alipoingia madarakani Machi 19, 2021 Rais Samia amekuwa akichukuwa jitihada mbalimbali za kuwavutia wawekezaji na kuhakikisha wale waliopo wanaendesha shughuli zao kwa kufuata sheria bila kubughudhiwa.

Na Ahmed Sagaff – MAELEZO

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments