Ujenzi barabara ya Kimara-Kibaha wafikia hatua za mwisho

MRADI wa upanuzi wa Barabara ya Morogoro sehemu ya Kimara-Kibaha kwa njia nane (kilomita 19.2), unaendelea vizuri na kwa sasa umefika asilimia 94.


Kwa mujibu wa taarifa zilizoonwa na DIRAMAKINI Blog,mradi huo unafadhiliwa na Serikali kwa asilimia mia moja na gharama yake ni takriban Shilingi Bilioni 161 huku ukitarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Desemba, mwaka huu.

Aidha, Serikali imeshamlipa Mkandarasi malipo ya zaidi ya shilingi bilioni 149. 8 ambazo ni sawa na asilimia 93 kulingana na kazi aliyoifanya.

Hadi sasa kazi zilizobakia ni kuweka taa za kuongozea magari, taa za kuangaza barabarani, kuweka kingo (kerbstobne) na kutenga njia zinazoelekea mjini na zinazotoka mjini na kumalizia lami kipande cha kilometa 4 kutoka eneo la Gogoni- Kibamba hadi Kibaha.

Mradi huu unatekelezwa na Serikali kupitia Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS), ambapo lengo lake kubwa ni kupunguza msongamano kwa wasafiri na wasafirishaji wanaongia katikati ya jiji la Dar es Salaam.

Aidha,kukamilika kwa mradi huu kutaunganisha nchi yetu na nchi jirani za Rwanda, Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Malawi.

Mradi huo ulianza mwaka 2018 na unajengwa na Kampuni ya kikandarasi ya Estim kutoka Tanzania.
 NA MWANDISHI MAALUM

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments