Chriss Mugalu wa Simba SC arejea nyumbani

Chriss Mugalu ambaye ni mshambuliaji wa mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Simba SC amerudi nchini kwao Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.


Mshambuliaji huo amerudi nyumbani kwa ajili ya kujiuguza huku akisema atarudi akiwa imara zaidi hapo baadae, Mungu akimjalia afya njema.

Mugalu alipata majeraha wakati Simba SC ikiwa kwenye maandalizi ya kucheza dhidi ya Jwaneng Galaxy ya Botswana mwezi uliopita ambapo hajarejea uwanjani tangu wakati huo.

Amesema, amelazimika kurudi nyumbani kwao ili apate muda wa kupumzika na kuendelea na tiba zaidi.

“Bado sijafahamu naweza kurejea wakati gani uwanjani , lakini matibabu ambayo nayafanya sasa ni ya hali ya juu na natakiwa kupumzika muda mwingi ndio maana nimerudi nyumbani,"amesema.

Mshambuliaji huyo alimaliza nafasi ya pili katika orodha ya wafungaji bora msimu uliopita 2020/21, akitanguliwa na mshambuliaji mwenzake wa Simba SC John Bocco.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments