SIMBA SC YAPATA ALAMA TATU DAKIKA ZA LALA SALAMA, YAICHAPA NAMUNGO 1-0

 

Klabu ya Simba Sc yafanikiwa kuondoka na alama tatu muhimu kwenye mchezo dhidi ya Namungo ambapo wameshinda 1-0 katika dimba la Benjamini Mkapa Jijini Dar es Salaam.

Mchezo huo ambao ulikuwa wa aina yake, kulishuhudiwa na kadi nyekundu kwa mchezaji wa Namungo Fc kiungo Abdulaziz Makame baada ya kumchezea rafu mbaya Shomari Kapombe.

Simba ilifanya mabadiliko ya wachezaji kadhaa ambao walichangia kwa kiasi kikubwa kupata matokeo mazuri.

Meddie kagere ndiye aliyeokoa jahazi mara baada ya kufunga kwa kichwa akipokea krosi kutoka kwa beki Mohamed Husein dakika ya 95 ya mchezo.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments