AJIBU ASAINI AZAM FC

  


NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Klabu ya Azam Fc imefanikiwa kuinasa saini ya Ibrahimu Ajibu akitokea klabu ya Simba Sc mara baada ya kuitumikia klabu hiyo kwa mafanikio makubwa.

Ajibu amekuwa miongoni mwa wachezaji wakipekee waliochezea timu kubwa mbili ambazo ni mahasimu yaani Simba Sc pamoja na Yanga.

Sasa Ajibu amejiunga na Azam Fc ili kuweza kuongeza nguvu kwenye kikosi hicho ambacho kimekuwa kikisuasua msimu huu.

Kupitia kwenye ukurasa wa klabu ya Simba Sc kwenye mitandao ya kijamii wamemtakia kila la heri mchezaji huyo kwa kuandika "Kwa maslahi ya pande zote mbili, uongozi wa klabu umefikia makubaliano na mchezaji Ibrahim Ajibu kusitisha mkataba wake kuanzia leo Alhamisi Desemba 30, 2021".

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments