MWENYEKITI WA CCM NA RAIS SAMIA KUONGOZA KIKAO CHA HALMASHAURI KUU YA CCM TAIFA JIJINI DODOMA

Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi Taifa itakutana Desemba 18, 2021 chini ya Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ndugu, Samia Suluhu Hassan.

Kikao hicho kitatanguliwa na vikao vya Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa na Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kuanzia Desemba 15, 2021.

Vikao vyote ni vya kawaida kwa mujibu wa Katiba ya CCM ya Mwaka 1977 toleo la Mwaka 2020 ibara ya 108 (2). Ambavyo vitafanyika Makao Mkuu ya Chama Cha Mapinduzi Jijini Dodoma ambapo maandalizi ya vikao hivyo yamekamilika.

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI.

SHAKA HAMDU SHAKA
KATIBU WA HALMASHAURI KUU
YA CCM TAIFA ITIKADI NA UENEZI.
14 DESEMBA, 2021.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments