RPC Manyara awataka wananchi waweke ulinzi kwenye sikukuu

Jeshi la polisi mkoani Manyara limewataka wananchi waweke ulinzi majumbani mwao ili kujilinda wakati huu wa sikukuu za mwisho wa mwaka, huku pia jeshi hilo likiimarisha ulinzi huo.

Kamanda wa polisi wa mkoa wa Manyara, kamishna msaidizi (ACP) Benjamin Kuzaga, ameyasema hayo mjini Babati Desemba 24 wakati akielezea mikakati ya ulinzi wa polisi kwenye sikukuu za mwisho wa mwaka.

Kamanda Kuzaga amesema katika kuelekea kwenye sikukuu za Christmas na mwaka mpya, pamoja na polisi kuwalinda watu wajitahidi kuwa walinzi wa mali zao wenyewe.

Amesema jukumu la ulinzi wa raia na mali zake siyo wa polisi pekee ni la jamii kwa ujumla hivyo wananchi nao wahakikishe wanaimarisha ulinzi majumbani mwao.

Pia, amewataka kutokaribisha ovyo watu majumbani ambao ni wageni wasiowafahamu kwani wengine ndiyo wanageuka kuwa wezi wa majumbani.


TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments