Mradi huu unajishghulisha na kuwajengea wanawake uwezo na kuwapa mitaji ya kuanzisha biashara ya pamoja ambayo wakinamama wenywe huchangia nusu ya mtaji na mradi unawaongezea nusu iliyobaki.
(Mratibu Wa Mradi Wa Kuwainua Wanawake Kiuchumi Mkoani Arusha) Bi Mesha Singolyo |
Hivyo Wakinamama huchangia M.3 na Sara naye huwapa 3M jumla zinakuwa 6 na wananunua ngombe Na Kuwanenepesha kwa miezi kadhaaa kisha kuwauza na kugawana faida, Fedha hizo ni ruzuku na sio deni wao kazi yao ni kula faida na kuzungusha mtaji.
Mratibu Mradi Wa Kuwainua Wakinamama Mkoani Arusha Bi Mesha Pius Singolyo ni mratibu wa mradi huu , Ambao katika kufunga mwaka 2021 wamefanya hafla fupi wilaya ya Monduli na kugawa 12 M kwa vikundi 4 vya wamama.
Mgeni Rasmi Mkuu Wa Wilaya Ya Monduli Akikabidhi Vikundi Pesa |
Baadhi Ya Wanakikundi Wakibudisha Mbele ya Mgeni Rasmi |
Pia Bi Mesha Singolyo Amesema Anategemea Kufika Wilaya Ngorongoro week Ijayo Ambapo Atagawa Milioni 9 Kwa Vikundi 3 Kata Ya Orbomba, Digodigo Na Sale.
Baada Ya Kupatiwa Pesa Vikundi Hivyo Huelekea Sokoni(Minadani) Kwajili Ya Kujipatia Ngombe Kwajili Ya Kuwaborsha na kuwa Fanyia Biaashara Ilikujiongezea Kipato Katika Vikundi Vyao
0 Comments