WAZIRI WA NCHI OFISI YA RAISI TAMISEMI MHE:UMMY MWALIMU AMEENDELEA NA ZIARA YAKE YA KIKAZI MKOANI SINGIDA

Waziri wa Nchi ofisi Ya Rais tamisemi Mhe. Ummy Mwalimu ameendelea na ziara yake ya kikazi mkoani Singida kwa kukutana na Sekretarieti ya Mkoa wa Singida na kupokea taaarifa ya mkoa, kujadili hali ya watumishi, utekelezaji wa miradi ya maendeleo, ukusanyaji wa mapato ya halmashauri na upelekaji wa fedha za mapato ya ndani kwenye miradi ya maendeleo.

Halkadhalika Mhe. Ummymwalimu amepokea changamoto mbalimbali zilizowasilishwa na Viongozi wa Mkoa huo na kuzitolea ufafanuzi.

Katika kikao hicho kwa pamoja wamekubalina namna bora ya Utekelezaji wa shughuli za Serikali katika Mkoa wa Singida.

Baada ya kikao hiki ataendelea na ziara yake katika Halmashauri ya Manispaa ya Singida kukagua miradi ya maendeleo na kikao na baraza la madiwani la Halmashauri hiyo.

 

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments