YANGA YAMALIZA MWAKA KWA KUICHAPA DODOMA JIJI 4-0

 Klabu ya Yanga imeichapa mvua ya magoli timu ya Dodoma Jiji mabao 4-0 katika mchezo wa NBC Premier league uliochezwa kwenye dimba la Benjamini Mkapa Jijini Dar es Salaam.


Yanga imecheza kandanda safi ambapo mshambuliaji wao mahiri Fiston Mayele alipachika bao la kuongoza dakika ya 42 kipindi cha kwanza .

Kipindi cha pili Yanga iliendelea kutawala mchezo kwani mpaka dakika ya 54 ya mchezo Yanga ilikuwa inatawala mchezo kwa asilimia 80% kwa 20%.

Yanga ilifanikiwakupata bao la pili kupitia kwa winga wao Jesus Muloko na baadae Dodoma Jiji kujifunga.

Aucho alifunga ubao wa magoli kwa kupachika bao tamu akipokea pasi kutoka kwa Jesus Muloko.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments