KATIBU WA BUNGE AANIKA MAJINA 9 YA WAGOMBEA USPIKA WA BUNGE WATAKAOPIGIWA KURA LEO BUNGENI

Katibu wa Bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania Nenelwa Mwihambi Akiongea na Waandishi wa Habari kuhusu kukamilika zoezi la uteuzi na utaratibu wa uchaguzi wa Spika wa Bunge.

KATIBU wa Bunge na msimamizi wa uchaguzi wa Spika Nenelwa Mwihambi(NDC) ametangaza kukamilika zoezi la uteuzi na utaratibu wa uchaguzi wa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jana Januari 31,2022 saa 10.00 jioni.


Akiongea na Waandishi wa habari jana Bungeni Dodoma,amesema zoezi hilo liliruhusu Wagombea ambao ni wabunge na wasio wabunge na kwamba kwa wagombea wenye vyama,vyama vyao  vilitakiwa kuwasilisha majina yao kwenye tume ya uchaguzi.


Amesema hadi sasa majina ya wagombea yaliyowasilishwa na kukidhi matakwa ya kisheria ni tisa ambapo miongoni mwa wagombea hao,nane sio wabunge na mmoja ni mbunge.


Sambamba na hayo ameyataja majina ya wagombea hao kuwa ni Abdullah Mohammed Said (NRA),Ivan Jackson Maganza (TLP),David Daud Mwaijojele (CCK),Georges Gabriel Busungu (ADA-Tadea),na Kunje Ngombale Mwiru.


Wengine ni Maimuna Said Kassim (ADC),Ndonge Said Ndonge (AAFP),Saidoun Abrahman Khatibu (DP) na Dkt. Tulia Ackson(CCM).


Aidha Katibu huyo wa Bunge amewataka wagombea hao kufika mapema Bungeni hapo leo na kwamba saa tatu asubuhi au muda mfupi baada ya hapo atawasilisha majina yao mbele ya wapiga kura ambao ni waheshimiwa wabunge .


Ametumia pia nafasi hiyo kuwashukuru wagombea wa vyama vyote vya siasa waliojitokeza ikiwa ni pamoja na kuipa ushirikiano wao Ofisi hiyo ya Katibu wa Bunge hadi zoezi hilo linakamilika.


Na Dotto Kwilasa 


TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments