KUHUSU SHABIKI ALIYEJIUA SIMBA SC IKICHAPWA NA MBEYA CITY

 


Baada ya Taarifa kusambaa kuwa Kijana Khalfan Mwambena (17) mkazi wa Jijini Mbeya na Shabiki kindaki ndaki wa Simba kusambaa kuwa amejiua baada ya Simba kupoteza mchezo dhidi ya Mbeya City.

Klabu ya Simba Kupitia Meneja wa Habari na mawasiliano wa Klabu hiyo, Ahmed Ally umekanusha taarifa hiyo na kueleza kuwa Shabiki huyo amefariki siku ya mchezo huo majira ya asubuhi kabla hata ya mchezo kuchezwa.

Sasa klabu ya Simba imekwenda mbali na kuthamini mapenzi ya Shabiki huyo kwa Klabu ya Simba. Simba imetoa taarifa kuonesha kuguswa na msiba wa shabiki huyo na kutoa pole kwa familia na Wanasimba kwa ujumla.

Tazama sehemu ya Taarifa ya Simba kwenda kwa Familia, Wapenzi, Wanachama na Mashabiki.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments