Maandamano kwa ajili ya kuachiliwa huru mfungwa wa kisiasa wa serikali ya Congo DRC


Maandamano yalifanyika jana Jumanne huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kwa ajili ya kushinikiza kuachiliwa huru mfungwa mashuhuri wa kisiasa wa serikali ya Kinshasa ambapo makumi ya watu walikeruhiwa katika maandamano hayo.

Maandamano hayo yalifanyika katika mji wa Lubumbashi ulioko kusini mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kwa ajili ya kushinikiza kuachiliwa huru Daniel Ngoy Mulunda, mkuu wa zamani wa Tume Huru ya Uchaguzi ya Congo kutoka mikononi mwa wafuasi wa Joseph Kabila, Rais wa zamani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, na ambaye (Mulunda) pia ni mpinzani wa serikali ya hivi sasa ya nchi hiyo.

Maandamano hayo yaliingiliwa kati na polisi ambayo iliyavunja na kupelekea makumi ya watu  kujeruhiwa.

Kufuatia ghasia zilizojiri baada ya polisi kuyavunja maandaamano, watu wasiopungua 50 wameripotiwa kujeruhiwa ambapo hali ya watu 14 kati yao inasemekana kuwa mbaya sana.


                                                                 

Waandamanaji wengine 10 wanaripotiwa kutiwa nguvuni na polisi.

Hii ni katika hali ambayo Moise Katumbi, mwanasiasa mashuhuri wa Kongo amelaani hatua ya polisi ya kutumia mabavu kuvunja maandamano hayo yaliyokuwa ya amani. Ngoy Mulunda alikamatwa na kuhukumiwa miaka mitatu jela kwa tuhuma za kuchochea ghasia na kueneza chuki nchini Congo.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments