MAYELE AZIDI KUKIWASHA, YANGA YAIZIMA COASTAL UNION 2-0

 

Klabu ya Yanga Sc imefanikiwa kuondoka na alama tatu mara baada ya kufanikiwa kuichapa Coastal Union ya Tanga kwa mabao 2-0 katika dimba la Mkwakwani Tanga.

Yanga Sc ilianza kupata bao katika kipindi cha kwanza kupitia kwa mshambuliaji wao raia wa DR Congo Fiston Mayele ambaye alimalizia krosi iliyopigwa na beki Djuma Shabani dakika ya 40 ya mchezo.

Goli la pili la Yanga liliwekwa kimyani na Said Ntibazokiza dakika ya 90 ya mchezo akipokea pasi murua kutoka kwa Farid Mussa.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments