Tukikamlisha zoezi la kuviwezesha vikundi saba 7 vya wamama wajasirimali wilaya ya Longido 11Jan 2022. Ambapo wamama hao wameweza kujipatia m 21 kama mitaji ya biashara zao.
Mesha Singolyo ambaye ni mratibu wa mradi huu wa wamama amesema silaha pekee ya kuondokana na umaskini ni wamama kuweza kukataaa kuwa tegemezi.
Hivyo amewaasa wanawake wa jamii ya kifugajii kufanya kazi kwa bidii na kujifunza nidhamu ya pesa kwa kuweka akiba kidogo ya wanachopata.
Kumiliki pesa inakupa nguvu ya kufanya maamuzi na kusimamia majukum yako kama mama kwa amani. kutokuwa tegemezi kuna leta afya ya ndoa, kunaongeza upendo kwenye familia kunaongeza utu, thamani na heshima ya mwanamke kwenye jamiii.
Kikundi Cha Wamama Kikipokea Pesa |
Wanafunzi Wakipokea Mahitaji Yao Ya shule |
0 Comments