SIMBA YATINGA FAINALI MAPINDUZI CUP, YAICHAPA NAMUNGO FC 2-0


KLABU ya Simba imefanikiwa kufuzu FAINALI katika michuano ya Mapinduzi Cup mara baada ya kuinyuka Namungo Fc mabao 2-0.

Simba Sc imefanikiwa kupata mabao yao kupitia kwa mshambuliaji wake Meddie Kagere pamoja na kiungo mshambuliaji wao raia wa Senegal Sakho ambaye ameonesha kuimarika kwa mechi za hivi karibuni.

Simba Sc rasmi itakutana na Azam Fc fainali ya Mapinduzi Cup ikiwa Azam Fc kufanikiwa kuwaondoa Yanga Sc kwa mikwaju ya Penati.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments