WASIOJULIKANA WAFUKUA KABURI NA KUTOWEKA NA MWILI WA MAREHEMU

                    Kaburi la mtoto Christian Samson lililofukuliwa

Mwili wa mtoto Christian Samson (1), aliyezikwa siku ya Jumapili katika makaburi ya kitongoji cha Kipondoda wilayani Manyoni mkoani Singida, umefukuliwa na kuchukuliwa na watu wasiojulikana licha ya ndugu kuutafuta bila mafanikio.

Simanzi na huzuni zilitawala katika makaburi hayo hii ikiwa sio mara ya kwanza vitendo hivyo vya ufukuaji wa makaburi kujitokeza, na mara hii imejitokeza hali isiyokuwa ya kawaida kwa kuwa mwili marehemu umetafutwa kwa zaidi ya saa nne huku jitihada hizo zikishindikana.

Kufuatia hali hiyo imemlazimu Mkuu wa wilaya ya Rahabu Mwagisa, na kuzungumzia vitendo hivyo huku akisisitiza suala la maombi kuwa ni la muhimu na jeshi la polisi linafuatilia ili kuwabaini waliohusika na kitendo hicho.

Chanzo - EATV

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments