Mkutano wa viongozi wa Umoja wa Ulaya na Afrika umeanza leo Brussels Ubelgiji


Mkutano wa viongozi wa Umoja wa Afrika na wa Umoja wa Ulaya umeanza leo katika mji mkuu wa Ubelgiji Brussels.

Viongozi hao wanakutana kwa ajili ya mazungumzo ya siku mbili kuanzia leo, wakiazimia kuimarisha ushirikiano, huku Ulaya ikiahidi uwekezaji mkubwa barani Afrika.

Mkutano wa mara hii una umuhimu wa aina yake kutokana na changamoto mbalimbali zinazolikabili bara la Afrika na mataifa ya Ulaya pia. Akihutubia katika mkutano huo, Josep Borrell, Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya amesema kuwa, bara la Ulaya linapaswa kuisaidia Afrika ili kuyashughulikia matatizo yake.

Uhusiano baina ya mabara hayo mawili umekuwa ukiingia dosari kutokana na matatizo mtawalia, yakiwemo usambazaji wa chanjo ya Covid-19, namna ya kuzuia uhamiaji haramu, wimbi la mapinduzi ya kijeshi barani Afrika na kadhalika Rais wa Senegal Macky Sall ambaye ni Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika amesema lengo la mkutano huu ni kufikia uhusiano mpya unaodhihirika kwa vitendo.

 

Huu ni mkutano wa sita wa aina yake ambapo zaidi ya wakuu 80 wa nchi na serikali wanashiriki katika mkkutano hhuo leo la kesho huku nusu yao wakitokea barani Afrika.

Katika miaka ya hivi karibuni, uhusiano wa Bara la Afrika na Umoja wa Ulaya umekumbwa na changamoto na hata mivutano tofautio kuhusiana na masuala mbaliambali.

Viongozi wa Afrika wamekuwa wakikosoa sera za baadhi ya mataifa ya Umoja wa Ulaya kwa bara la Afrika huku baadhi ya mataifa hayo yakiamiliana na nchi za Kiafrika kama koloni lao.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments